Simbachawene aipongeza Bodi ya Wakurugenzi e-GA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mb), ameipongeza Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa usimamizi mzuri wa taasisi hiyo. Mhe. Waziri ameyasema hayo Mei 20, mwaka huu wakati alipofanya kikao kazi maalum na bodi hiyo katika ofisi za e-GA Mtumba jijini Dodoma. Aliongeza kuwa, usimamizi makini wa bodi hiyo umeiwezesha e-GA kutekeleza majukumu y...