Mhe. Ridhiwani Aipongeza e-GA Ujenzi wa Mifumo Bunifu

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb), ameipongeza Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa juhudi zake za kuendelea kujenga Serikali kidijitali kupitia mifumo mbalimbali inayorahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuongeza ufanisi katika taasisi za umma. Mhe. Ridhiwani ametoa pongezi hizo alipofungua Mkutano wa Pili wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Rasilimaliw...







