eMrejesho V2 YACHAGULIWA KUWANIA TUZO ZA WSIS 2025

Mfumo wa eMrejesho toleo la pili (eMrejeshoV2) kutoka Tanzania,umechaguliwa kuwania Tuzo za Mkutano wa Dunia wa Jumuiya ya TEHAMA mwaka 2025 (World Summit on the Information Society -WSIS 2025). Tuzo hizi hutolewa na WSIS, kwa uratibu wa Shirika la Mawasiliano la Umoja wa Mataifa (International Telecommunications Union - ITU), kwa lengo la kutambua na kuchochea miradi bunifu, inayotumia TEHAMA katika kuchangia maendeleo endelevu duniani. Mf...