MFUMO WA e-Mrejesho WASHINDA TUZO YA UMOJA WA MATAIFA YA UBUNIFU KATIKA HUDUMA ZA UMMA

Tanzania imeshinda tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Ubunifu katika Huduma za Umma kwa mwaka 2024 ‘UN Public Service Innovation Awards’ kupitia mfumo wa e-Mrejesho, ambao umetambuliwa na umoja huo kama jukwaa linalowezesha serikali kukusanya maoni na malalamiko ya wananchi kwa njia ya kidijitali, na hivyo kufanya maamuzi ya sera na utekelezaji kwa wakati.Hafla ya utoaji wa tuzo za Umoja wa Mataifa kuhusu Huduma za Umma imefanyika Juni 26 mwaka huu waka...







