MIFUMO YA KIELEKTRONIKI YATAJWA KUZUIA UPOTEVU WA MAPATO YA SERIKALI

Matumizi sahihi na salama ya mifumo ya kieletroniki Serikalini, yametajwa kuwa suluhisho la kudumu katika kuziba mianya ya upotevu wa rasilimali za serikali ikiwemo mapato yatokanayo na vyanzo mbalimbali nchini.Hayo yameelezwa jana jijini Dodoma na Waziri wa Fedha Dkt Mwigulu Nchemba, wakati akipokea na kuzindua Mfumo wa Kieletroni wa Kuratibu Ununuzi wa Mafuta Serikalini, ujulikanao kama ‘GPSA Intergrated Management Information System’ (GIMIS),...