Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA wametakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Miongozo na Viwango vya Serikali Mtandao

Wakuu wa Vitengo vya TEHAMA wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Kilimo, wametakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Miongozo na Viwango vya Serikali Mtandao katika kusanifu miradi ya TEHAMA ili kuhakikisha inaleta tija katika sekta ya kilimo.Wito huo umetolewa leo na Afisa TEHAMA kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Bw.George Bagomwa, wakati akiwasilisha mada kuhusu utekelezaji wa miradi ya TEHAMA Serikalini, kwenye kikao kazi cha Wakuu wa Viteng...







