e-UKAGUZI: KUONGEZA UFANISI KATIKA SEKTA YA UKAGUZI NCHINI

Utekelezaji wa Jitihada za Serikali Mtandao, unategemea uwepo wa mfumo imara wa ukaguzi utakaoboresha na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kaguzi mbalimbali zinazofanywa na wakaguzi ndani na nje ya Taasisi za Umma.Mfumo mpya wa kaguzi ujulikanao kama e-Ukaguzi ni mfumo unaosaidia na kuimarisha utendaji kazi wa kaguzi za ndani za Taasisi za Umma, ikiwemo kuandaa mpango kazi wa mwaka, kutekeleza kaguzi, kufanya ufuatiliaji wa hoja mbalimbali...







