MRADI WA ‘DIGITAL TANZANIA’ KUIMARISHA HUDUMA ZA KIDIJITALI NCHINI

Mradi wa ‘Digital Tanzania’ unatarajiwa kuimarisha utoaji wa huduma kwa njia ya kidijitali kati ya Serikali, Wananchi pamoja na Wafanyabiashara sambamba na kuchochea uwekezaji katika miradi ya kidijitali nchini.Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Eng. Benedict Ndomba alipozungumza na mwandishi wetu kuhusu mradi huo ofisini kwake jijini Dodoma.Alibainisha kuwa, mradi huo una malengo makuu mawili ambayo ni ku...







