TAASISI ZA UMMA ZAHIMIZWA KUENDESHA VIKAO KWA NJIA YA MTANDAO KUPUNGUZA GHARAMA

Meneja Mawasiliano Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Bi. Subira Kaswaga, amezitaka Taasisi za Umma nchini kuendesha vikao kidijitali kwa kutumia mfumo wa e-Mikutano ili kupunguza gharama za uendeshaji wa vikao. Kaswaga alitoa rai hiyo jana, alipofanya mazungumzo na mwandishi wetu ofisini kwake jijini Dodoma kuhusu faida zitokanazo na mfumo wa e-Mikutano. Alibainisha kuwa, mfumo wa e-Mikutano unawawezesha watumishi wa Taasisi za umma kufan...