e-GA NA MIKAKATI YA KUKUZA SERIKALI YA KIDIJITALI

Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) imetaja mikakati mbalimbali iliyojiwekea ili kujenga Serikali ya kidijitali kwa kuhahikisha kuwa, Taasisi za Umma zinatoa huduma kwa wananchi kwa njia ya dijitali.Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Meneja wa Usimamizi wa Uzingatiaji wa Viwango vya Serikali Mtandao wa Mamlaka Bi. Sultana Seiff, wakati akiwasilisha mada kuhusu Utoaji wa Huduma kwa Umma Kidijitali bila Kumuacha Mtu Nyuma (‘leaving no one behind...







