Sheria na Kanuni za Serikali Mtandao (Serikali ya Kidigitali) zinasaidia Matumizi Sahihi ya TEHAMA Serikalini

Taasisi za umma zimeaswa kuzingatia sera, sheria, kanuni, viwango na miongozo ya serikali mtandao wakati wa kusanifu, kujenga na kuendesha mifumo na miundombinu ya TEHAMA kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa umma.Hayo, yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Dkt. Jabiri Kuwe Bakari leo Septemba 25, 2020 jijini Dodoma mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya kujenga uelewa kuhusu Sheria ya Serikali M...







