emblem
Mamlaka ya Serikali Mtandao
TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO/IEC 27001:2022 | ISO 9001: 2015
ega Logo
Habari
ega-svg-tree

Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano wa Serikali, wametakiwa kutumia mifumo ya Serikali katika mawasiiano, ili kulinda usalama na usiri wa taarifa za Serikali. Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Huduma za TEHAMA wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Bw. Ricco Boma, wakati akichangia mada kuhusu mabadiliko ya teknolojia katika mawasiliano, kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano wa Ser...

Soma Zaidi

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango, amezielekeza taasisi za umma kuwasiliana na kubadilishana taarifa kidijitali, ili kurahisisha utendaji kazi katika taasisi zao na utoaji wa huduma za Serikali kwa wananchi kwa urahisi na gharama nafuu zaidi. Dkt. Mpango amesema hayo leo, wakati akifungua Kikao Kazi cha 5 cha Serikali Mtandao, kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha...

Soma Zaidi

Sasa ni Jumuishi uratibu wa makongamano na Semina ni rahisi zaidi Mfumo wa Uratibu, Usimamizi na Uendeshaji wa Mafunzo na Semina (Training and Seminar Management System - TSMS), toleo la pili (version 2) umeboreshwa zaidi ili kuongeza ufanisi wa uendeshaji, usimamizi na uratibu wa mafunzo na semina, katika taasisi za umma. Mfumo huu kwa sasa umeongezewa moduli sita kutoka moduli nane za awali na kufanya jumla ya moduli 14, zinazomuweze...

Soma Zaidi

Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuuona Mwaka Mpya wa 2025, kwa niaba ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), napenda kuwatakia nyote Heri ya Mwaka Mpya 2025. Mamlaka ya Serikali Mtandao, inapenda kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuiwezesha e-GA kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Katika mwaka uliopita (2024), e-GA imeweza kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kuratibu,...

Soma Zaidi

Takriban wadau 1000 wa serikali mtandao wanatarajiwa kukutana kwa siku tatu, kuanzia Februari 11 hadi 13, 2025 jijini Arusha, ili kujadiliana kuhusu hali ya utekelezaji wa Serikali Mtandao nchini, kuainisha changamoto, sambamba na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto hizo. Wadau hao kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali ya umma, wanatarajiwa kukutana katika Mkutano (5) wa mwaka wa Serikali Mtandao, utakaofanyika katik...

Soma Zaidi
Mpangilio