e-GA NA MKAKATI WA KUIBUA NA KUKUZA VIPAJI VYA VIJANA WAZAWA KATIKA ENEO LA TEHAMA

“Uadilifu na ubunifu kwa utoaji wa huduma bora kwa umma” huu ndio moto wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), unaoangaza njia inayochochea bunifu mbalimbali za TEHAMA zitakazosaidia kuboresha utoaji wa huduma za Serikali kidijitali.Ili kufikia mafanikio haya, Oktoba 2019 e-GA ilianzisha Kituo cha Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Serikali Mtandao (eGOVRIDC), kwa lengo la kuimarisha na kukuza tafiti pamoja na bunifu za TEHAMA, kwa kushirikiana na...