e-GA YAPONGEZWA UJENZI WA MIFUMO YA KIELEKTRONIKI SERIKALINI

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Clement Sangu (Mb), ameipongeza Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), kwa kutengeneza mifumo ya kielektroniki ya ukusanyaji wa fedha za Serikali ambayo imesaidia kuzuia upotevu wa fedha za umma. Mhe. Sangu amesema hayo Septemba 05 mwaka huu, wakati alipotembelea Makao Makuu ya Ofisi za e-GA zilizopo Mtumba jijini Dodoma, na kufanya mazungumzo na watumishi wa e...







