ZINGATIENI SHERIA YA SERIKALI MTANDAO MNAPOFANYA UKAGUZI WA MIFUMO YA TEHAMA: MWAMNYASI

Wakaguzi wa Ndani katika taasisi na mashirika ya umma wametakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao katika ukaguzi wa miradi na mifumo ya TEHAMA ili kulinda thamani halisi ya fedha za Serikali katika miradi hiyo. Rai hiyo imetolewa jana na Mkurugenzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi anayeshughulikia Wizara, Idara zinazojitegemea na Mamlaka za Serikali, kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali (IAG) Bw...







