WANAFUNZI KUTOKA KITUO CHA UTAFITI NA UBUNIFU WATEMBELEA MAKAO MAKUU YA e-GA

Wanafunzi 55 kutoka Vyuo Vikuu 11 nchini waliopo katika programu maalumu ya mafunzo kwa vitendo inayoendeshwa na Kituo cha Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Serikali Mtandao (e-GovRIDC) wametembelea Makao Makuu ya e-GA yaliyopo Mtumba jijini Dodoma Septemba 08, 2023. Akipokea ugeni huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mkurugenzi wa Huduma na Uwezeshaji wa e-GA Bw.Salum Mussa amewataka vijana hao kutumia uzoefu walioupata katika kituo hicho kubun...







