e-GA KUIMARISHA MAHUSIANO NA CHUO KIKUU CHA MZUMBE

Mamlaka ya Serikali Mtanda (e-GA) inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na Chuo Kikuu cha Mzumbe kupitia mkataba wa makubaliano (MOU) unaotarajiwa kufanyiwa maboresho hivi karibuni. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa e-GA Eng. Benedict Ndomba, wakati wa kikao cha Pamoja kati ya e-GA na Chuo Kikuu cha Mzumbe kilichofanyika leo katika ofisi za e-GA jijini Dodoma, kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa mkataba wa kwanza wa makubaliano (MOU)....







