WAKAGUZI WA NDANI WAHIMIZWA KUZINGATIA SHERIA YA SERIKALI MTANDAO KWENYE UKAGUZI WA MIRADI YA TEHAMA

Wakaguzi wa Ndani katika Taasisi za Umma wametakiwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, wakati wa ukaguzi wa miradi na mifumo mbalimbali ya TEHAMA kwenye taasisi zao, ili kuhakikisha wanatenda haki.Wito huo umetolewa na Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali CPA. Paison Mwamnyasi, wakati wa ufunguzi wa awamu ya nne ya mafunzo maalum kuhusu ukaguzi wa mifumo na miradi ya TEHAMA...







