MHE. NDEJEMBI AZITAKA TAASISI ZA UMMA KUSHIRIKIANA NA e-GA

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb) amezitaka Taasisi za Umma kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) katika kutengeneza Mifumo ya TEHAMA itakayorahisisha utoaji wa huduma bora kwa Wananchi.Ndejembi alisema hayo jana, wakati alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja kukagua utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Mamlaka, katika Ofisi za e-GA Kanda ya Nyanda za Juu Kusin...