SIMBACHAWENE: TUTAHAKIKISHA MATUMIZI YA TEHAMA SERIKALINI YANAZIDI KUIMARIKA

Serikali imeahidi kuendelea kusimamia na kuhakikisha matumizi ya TEHAMA katika Taasisi za Umma yanaimarika zaidi, ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na kurahisisha upatikanaji wa huduma za Serikali kwa wananchi kidijitali.Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mh. George Simbachawene, wakati akifungua Kikao Kazi cha 4 cha Serikali Mtandao kilichofanyika kwa siku tatu kuanzia Februar...