TAASISI ZA UMMA ZAIDI YA 80 ZIMEJIUNGA NA MFUMO WA KUBADILISHANA TAARIFA (GovESB)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mha. Benedict Ndomba, amesema kuwa zaidi ya taasisi za umma 80 zimejiunga katika Mfumo wa Ubadilishanaji Taarifa Serikalini (Government Enterprise Service Bus-GovESB).Ndomba alisema hayo wakati aliposhiriki mahojiano katika kipindi cha Adhuhuri lounge cha UTV Septemba 18, kuhusu jitihada za Mamlaka katika kuhakikisha mifumo ya TEHAMA Serikalini inawasiliana na kubadilishana taarifa.“Kuanzia mw...







