KATIBU MKUU - UTUMISHI AWAHIMIZA WATUMISHI WA e-GA KUWA WAADILIFU

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi, amewataka watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kulinda maslahi ya taifa. Mkomi alitoa kauli hiyo hivi karibuni, wakati wa kikao kazi cha watumishi wa e-GA na viongozi wa Wizara kilicholenga kujadili utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka. Alisema kuwa, watumishi wa e-GA wanashiriki katika kazi muhimu z...







