WAKAGUZI WA NDANI WATAKIWA KUZINGATIA VIWANGO NA MIONGOZO YA SERIKALI MTANDAO KATIKA MIRADI YA TEHAMA

Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Hesabu za Serikali (IAG) Mwanyika Semroki, amewataka Wakaguzi wa Ndani kuhakikisha Mifumo ya TEHAMA inayoanzishwa katika Taasisi zao inazingatia miongozo na viwango vilivyowekwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA).Mwanyika alitoa kauli hiyo jana wakati akifunga mafunzo maalum ya ukaguzi wa Mifumo na Miradi ya TEHAMA yaliyotolewa kwa Wakaguzi wa Ndani wa halmashauri na Tawala za Mikoa yaliyofanyika kwa siku tano mk...







