e-MREJESHO NI SULUHISHO LA KERO ZA WANANCHI

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), imetengeneza Mfumo wa kidigitali ujulikanao kama e-Mrejesho, unaomuwezesha mwananchi kuwasilisha malalamiko, kero, maoni, mapendekezo, au maulizo moja kwa moja kwenye Taasisi /Wizara husika sambamba na kufuatilia utekelezaji wake.Mfumo huo wa kidigitali una lengo la kumsaidia mwananchi kupunguza gharama pamoja na kuokoa muda wa kutembea umb...







