MIUNDOMBINU BORA NA SHIRIKISHI YA TEHAMA NI MUHIMU KATIKA KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA KWA UMMA

Serikali inaweka Miundombinu salama ya TEHAMA inayoziwezesha Taasisi za Umma kushirikiana katika matumizi ya rasilimali za TEHAMA ili kuondoa urudufu, kupunguza gharama na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa umma, pamoja na kuhakikisha usalama wa mawasiliano.Miundombinu iliyopo ni pamoja na Mkongo wa Taifa (NICTBB), Mtandao wa Serikali (GovNet), Vituo vya Kitaifa vya Data na Masafa ya Intaneti. Hayo yameelezwa na Meneja Usimamizi wa Mtandao...







