WAKUU WA IDARA NA VITENGO VYA TEHAMA SERIKALINI WAASWA KUWASHIRIKISHA WAKAGUZI WA NDANI KATIKA UJENZI WA MIFUMO YA TEHAMA

Wakuu wa Vitengo na Idara za TEHAMA Serikalini, wametakiwa kuwashirikisha Wakaguzi wa Ndani wa taasisi, katika hatua za awali za ujenzi wa mifumo na miradi ya TEHAMA ili kuhakikisha inazingatia Sheria, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao. Wito huo umetolewa jana Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali Bw. Benjamin Magai, wakati wa kufunga mafunzo maalum kwa Wakaguzi wa Ndani wa taasisi na mashirika ya u...