Mahakama ya Tanzania kutumia Mfumo wa Ofisi Mtandao katika Utendaji kazi

Mahakama ya Tanzania imejipanga kuanza rasmi matumizi ya Ofisi Mtandao (e-Office) kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi na kuhakikisha kuwa ndoto ya kuwa Mahakama Mtandao (e-Judiciary) inatimia. Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel Katika kikao chake cha kwanza na Menejimenti ya Mahakama kilichofanyika Agosti 23, 2021. Kikao hiki ni cha kwanza na Menejimenti baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Rais...







