Serikali Yasisitiza Uwekezaji Katika Mafunzo ya Teknolojia kwa Watumishi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameitaka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kuwajengea uwezo watumishi wake katika matumizi ya teknolojia zinazochipukia, ili kuhakikisha zinatumika kwa usalama na kuleta tija inayokusudia. Mhe. Ridhiwani ametoa rai hiyo Novemba 25 mwaka huu, alipozungumza na watumishi wa e-GA wakati alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Mamlaka hiy...







