ONGEZENI KASI YA MATUMIZI YA TEHAMA: SIMBACHAWENE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mb), amezitaka Taasisi za Umma zenye kiwango kidogo cha utekelezaji wa Jitihada za Serikali Mtandao, kuongeza kasi ya matumizi ya TEHAMA ili kuleta tija katika utendaji kazi wao. Mhe.Simbachawene ametoa kauli hiyo Februari 13 mwaka huu, wakati akifunga Kikao Kazi cha 5 cha Serikali Mtandao kilichofanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi...