emblem
Mamlaka ya Serikali Mtandao
TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015
ega Logo
Habari
ega-svg-tree

MAMLAKA ya Serikali Mtandao (e-GA), imetoa tuzo mbalimbali kwa Taasisi za Umma zilizofanya vizuri katika utekelezaji wa jitihada za Serikali Mtandao kwa mwaka wa fedha 2023/2024, ikiwa ni miongoni mwa mikakati ya kuchochea matumizi ya TEHAMA Serikalini. Tuzo hizo zilitolewa Februari 13 mwaka huu na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene (Mb), wakati akifunga Kikao kazi cha 5 cha...

Soma Zaidi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mb), amezitaka Taasisi za Umma zenye kiwango kidogo cha utekelezaji wa Jitihada za Serikali Mtandao, kuongeza kasi ya matumizi ya TEHAMA ili kuleta tija katika utendaji kazi wao. Mhe.Simbachawene ametoa kauli hiyo Februari 13 mwaka huu, wakati akifunga Kikao Kazi cha 5 cha Serikali Mtandao kilichofanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi...

Soma Zaidi

Mamlaka ya Serikali Mtandao(e-GA), imeandaa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo Wachambuzi wa Mifumo ya TEHAMA wa taasisi mbalimbali za umma. Mafunzo hayo ya siku 5 yanatolewa na kampuni ya kimataifa ya Koenig Solutions, yanalenga kuwajengea uwezo maafisa hao katika sekta ya ujenzi na uchambuzi wa mifumo ya TEHAMA katika taasisi zao. Katika mafunzo hayo yanayoendelea Kibaha mkoani Pwani, pia yameshirikisha maafisa kutoka baadhi ya Taasisi za...

Soma Zaidi

Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano wa Serikali, wametakiwa kutumia mifumo ya Serikali katika mawasiiano, ili kulinda usalama na usiri wa taarifa za Serikali. Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Huduma za TEHAMA wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Bw. Ricco Boma, wakati akichangia mada kuhusu mabadiliko ya teknolojia katika mawasiliano, kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano wa Ser...

Soma Zaidi

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango, amezielekeza taasisi za umma kuwasiliana na kubadilishana taarifa kidijitali, ili kurahisisha utendaji kazi katika taasisi zao na utoaji wa huduma za Serikali kwa wananchi kwa urahisi na gharama nafuu zaidi. Dkt. Mpango amesema hayo leo, wakati akifungua Kikao Kazi cha 5 cha Serikali Mtandao, kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha...

Soma Zaidi
Mpangilio