MAKALA: Mapinduzi ya Kidigitali Mahakamani: Hukumu sasa Zaandikwa kwa Akili Unde

Katika hatua inayotajwa kama mapinduzi ya kihistoria kwenye utoaji wa haki, Mahakama ya Tanzania imeanza kutumia Akili Unde (AI) katika uandishi wa hukumu, hatua inayorahisisha, kuharakisha na kuongeza uwazi wa mashauri huku ikiimarisha imani ya wananchi kwa mhimili huo wa dola. Akizungumza katika Kikao Kazi cha sita cha Serikali Mtandao kilichofanyika jijini Arusha Februari 17 hadi 19, 2026, Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabri...







