IMARISHENI UADILIFU KAZINI: MHANDISI NDOMBA

Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), wametakiwa kuimarisha na kuendeleza uadilifu kazini ili kuhakikisha Mamlaka inatekeleza majukumu yake kwa weledi na ufanisi zaidi. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Benedict Ndomba Februari 26 mwaka huu, wakati akifungua kikao cha wafanyakazi wa Mamlaka kilichofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam. Alisema kuwa, ili Mamlaka iendelee kut...