emblem

Mamlaka ya Serikali Mtandao

Uadilifu na Ubunifu kwa Utoaji Huduma Bora kwa Umma
TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

Taasisi Zahimizwa Kuwasilisha Taarifa za Miradi ya TEHAMA


Taasisi Zahimizwa Kuwasilisha Taarifa za Miradi ya TEHAMA


Hayo yamesemwa na Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala Bi. Suzan Mshakangoto kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi ya Wakala Juni 2, 2016.

Amesema baadhi ya vigezo vya mradi ni kuonesha jinsi gani utaboresha utendaji kazi wa taasisi husika, utoaji wa huduma kwa umma ikilinganishwa na utaratibu wa zamani na iwapo unatimiza malengo ya Dira ya Taifa ya Mandeleo 2025 na unazingatia Sera, Viwango, Miongozo na Taratibu za Serikali.

Ameeleza kuwa, taasisi za umma zimekuwa na miradi ya TEHAMA ambayo inafanana na hivyo kuiongezea Serikali gharama ya kuiendesha miradi hiyo jambo ambalo limekuwa na changamoto kubwa kwa Serikali.

Vilevile amesema, Wakala itahakikisha taasisi za umma zinakuwa na mifumo inayoongea, inayobadilishana taarifa na inayozingatia teknolojia iliyopo ili kuweza kukidhi mahitaji ya Serikali na kuboresha utoaji huduma kwa umma.

Wakala ya Serikali Mtandao (eGA), iliyoanzishwa 2012, ni taasisi ya Serikali yenye majukumu na mamlaka ya kuratibu, kusimamia na kukuza jitihada za Serikali Mtandao nchini Tanzania. Pia Wakala hii inasimamia udhibiti wa viwango vya Serikali Mtandao kwa kutumia Miongozo mbalimbali na Viwango vilivyowekwa ili kuwa na mifumo bora ya TEHAMA Serikalini.