emblem

Mamlaka ya Serikali Mtandao

Uadilifu na Ubunifu kwa Utoaji Huduma Bora kwa Umma
TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

Ziara ya Katibu Mkuu OR-MUU katika Ofisi za eGA


Ziara ya Katibu Mkuu OR-MUU katika Ofisi za eGA


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. George D. Yambesi, ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Wakala ya Serikali Mtandao ili kuboresha huduma na kusaidia kukuza jitihada zinazofanywa na Serikali Mtandao.

Amesema hayo katika ziara yake aliyofanya katika Ofisi ya Wakala ya Serikali Mtandao zilizopo  Jengo la TTCL  mtaa wa samora jijini Dar es salaam Februari 9, 2015.

Naye Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Hab Mkwizu, aliyeambatana na Katibu Mkuu pamoja na menejimenti ya Utumishi wa Umma ameshauri Wakala kujitangaza zaidi ili jamii ipatae kujua huduma zake na shughuli inazozifanya katika kuboresha huduma zinzaotolewa na Serikali kwa njia ya mtandao.

“Ninawashauri mjitangaze kwenye vyombo vya Habari ili jamii iwafahamu na kutambua huduma zote mnazozitoa pamoja na jitihada zote za Serikali Mtandao katika kukuza teknolojia ya Habari na Mawasilano” Alisema Bw. Mkwizu.